UDUNISHAJI WA KIJINSIA KATIKA LUGHA YA KISWAHILI NA ATHARI YAKE KATIKA MAENDELEO YA JAMII

Authors

  • Caroline Asiimwe

Abstract

Dhana ya udunishaji wa kijinsia inahusu hali ya kuwakweza na kuwatweza mwanamume au mwanamke. Hali hii inatokana na jinsi lugha inavyowasilisha itikadi ya jinsia na namna inavyochangia kukweza na kutweza mwanamke na mwanamume katika jamii. Makala hii inafafanua namna lugha ya Kiswahili inavyoendeleza udunishaji wa kijinsia kwa kumtweza mwanamke huku mwanamume akikwezwa kutokana na itikadi ya kijamii na kijinsia pamoja na kuelezea athari yake katika maendeleo ya jamii. Kwa kuwa Kiswahili ni lugha ya mawasiliano mapana, makala hii inahoji kwamba matumizi yake katika kuzuia udunishaji wa kijinsia ni ya mustakabali mzuri. Ili kupata maendeleo katika jamii, makala hii inapendekeza lugha ya Kiswahili iangaliwe kama rasilimali muhimu katika maendeleo na kuitumia kama zana ya kijamii ambayo ni tendaji. Hali hii itaimarisha mawasiliano bora yanayozingatia upya namna itikadi za kijamii zinavyowasilishwa kwa kutumia lugha yenye ubunifu na uvumbuzi ili kuakisi masuala ambayo yanalenga maendeleo.

Chakama

Downloads

Published

2022-04-12

Issue

Section

Journals