MATAPO YA UJAALA KATIKA JAMII ZA WATANZANIA
Keywords:
Falsafa, Falsafa-Tamaduni, UjaalaAbstract
Makala hii inahusu ujaala. Dhana ya ujaala tunaitumia humu kumaanisha nguvu au kani inayotawala matukio yote yanayowatokea viumbe pasi na wao kuwa na uwezo wa kuzuia, kubadili, wala kudhibiti. Hoja kuu ya makala ni kutanabaisha kwamba mwanadamu razini huitambua, kuikiri na kuitumia kani hii katika kuviendesha vipengele mbalimbali vya maisha yake. Makala hii yenye mwegamo wa utamaduni inatokana na uchunguzi mpana wa utamaduni wa Watanzania. Data zilipatikana kupitia usomaji wa nyaraka pamoja na usaili. Makala imeundwa na sehemu kuu nne: Utangulizi, chimbuko na maendeleo ya dhana ya ujaala, matapo ya ujaala, na hitimisho. Makala inafafanua matapo makuu mawili ya ujaala ambayo jamii za Watanzania huyatumia pamoja na vijenzi vyake. Tapo la kwanza lililofafanuliwa ni ujaala wa kijadi. Vijenzi vya tapo hili ni makaburi, hirizi, milima, miti mikubwa, mapango pamoja na mkusanyiko wa maji mengi. Tapo la pili ni ujaala wa kisasa. Hili limegawanyika katika vijitapo vya ujaala wa Kikristo (vijenzi vyake ni Nabii Yesu Kristo, taasisi ya kanisa, na Biblia), ujaala wa Kiislamu (vijenzi vyake ni Mtume Muhammad, hadithi, msikiti, na Kur’an) pamoja na Ujaala wa
Kihindu (vijenzi vyake ni wanyama kama vile ng’ombe.