ISIMU YA KIJANI YA MAJINA YA MIEZI KATIKA RUKIGA

Authors

  • Leonard Chacha Mwita
  • Aidah Mutenyo
  • Martin Mulei

Keywords:

mwezi, lugha, mazingira, isimu ya kijani, ikolojia

Abstract

Lugha haipatikani katika ombwe. Lugha ni matokeo ya mtagusano baina ya watu wanaoizungumza na mazingira yao. Kwa kweli, kuna uhusiano mkubwa baina ya mazingira, lugha na wazungumzaji wake. Makala hii itajikita katika majina ya kiasili na majina ya kisasa ya miezi ya mwaka katika Rukiga. Rukiga ni lugha ya Kibantu inayozungumzwa Kusini Magharibi mwa nchi ya Uganda, hasa eneo la Kabale. Majina asili ya miezi ya Rukiga yametokana na mahusiano ya watu na mazingira yao na yanaonyesha namna lugha inavyoweza kutumiwa kuzungumzia mazingira na kumwezesha binadamu kuyatawala. Majina haya ya kiasili yanaeleza mengi kuhusu mazingira na hali ya miezi husika. Katika utafiti huu, juhudi zilifanywa kubaini ikiwa matumizi ya majina ya ‘kisasa’ yanaakisi mabadiliko katika jamii kuhusu mtazamo wao juu ya mazingira. Uchunguzi huu uliongozwa na nadharia ya Filosofia ya Ikolojia (Ecosophy). Uchanganuzi uliofanywa unaonyesha kwamba majina ya ‘kisasa’ ya miezi yanadhihirisha ukosefu wa mtagusano kati ya wazungumzaji na mazingira kama ilivyokuwa katika majina ya kiasili. Makala inapendekeza mbinu mbalimbali za kuwezesha kizazi cha sasa kuyafahamu na kuyatumia majina ya asili ya miezi ya mwaka.

Chakama

Downloads

Published

2022-04-12

Issue

Section

Journals