FAHARASA KATIKA DIWANI ZA SAID AHMED MOHAMED: VIJENZI NA TIJA ZAKE

Authors

  • Hassan R. Hassan Hassan

Abstract

Makala hii inajadili faharasa katika diwani za Said Ahmed Mohamed kwa kuangazia vijenzi na tija zake. Faharasa ni sehemu muhimu katika vitabu vya fani mbalimbali. Sehemu hii aghalabu hujumuisha maneno magumu yaliyotumiwa ndani ya kitabu husika. Kupitia faharasa, wasomaji wamekuwa wakifaidika kwa kupata ufafanuzi wa maneno yaliyotumika kitabuni. Makala hii imetokana na uchunguzi wa kimaktaba. Mjadala unafanywa kwa kuegemezwa katika diwani tatu za Said Ahmed Mohamed ambazo ni ‘Sikate Tamaa’ (1980), ‘Kina cha Maisha’ (1984) na ‘Jicho la Ndani’ (2002). Matokeo ya uchunguzi yameonesha kuwa faharasa katika diwani teule zinaundwa na: maneno ya kilahaja, maneno ya kale na maneno ya kishairi. Aidha, kuna maneno yaliyogeuzwa kuwa na sura ya kizamani, vikasiri na mazidadi. Pia, uchunguzi umezibaini tija ziletwazo na faharasa hizo kuwa ni kupevusha taaluma ya leksikografia, kuhifadhi msamiati wa lugha, kufundisha lugha na kuonesha namna bora ya kufanya ukiushi katika ushairi. Aidha, faharasa huonesha ukwasi na umbuji wa lugha wa mtunzi na hujenga uhusiano wa mtunzi na jamii yake.

Chakama

Downloads

Published

2022-04-12

Issue

Section

Journals