MCHANGO WA RUNUNU KATIKA MAENDELEO YA KISWAHILI
Keywords:
rununu/simu tamba, simuwaya, simumtelezoAbstract
Kiswahili ni lugha inayokua na kusambaa katika maeneo mbalimbali ulimwenguni tena kwa kasi sana. Siku za hivi karibuni, nchi nyingi barani Afrika (zikiwemo Afrika Kusini, Rwanda, na Zimbabwe) zimeamua Kiswahili kifundishwe katika shule za nchi hizo, na zingine zimekubali Kiswahili kiwe mojawapo ya lugha rasmi za nchi (Rwanda). Kwa upande mwingine, matumizi ya rununu yameenea kwa mapana na marefu, hususan kutokana na upenyaji, kukubalika, na matumizi yake. Asilimia kubwa ya raia wa nchi ambapo Kiswahili kinatumika ama wanamiliki simu tamba au/na wana uwezo wa kutumia simu tamba katika maisha yao ya kila siku (kama vile matumizi ya huduma ya M-Pesa). Makala hii inahoji kuwa upatikanaji na matumizi ya rununu kwa wingi huchangia maendeleo ya jamii husika pamoja na yale ya Kiswahili. Itaangalia kwa kifupi historia ya simu tamba nchini Kenya, pamoja na kuchunguza namna raia wa nchi husika wanavyoingiliana na kuhusiana na rununu na, ikiwa wanatumia Kiswahili katika rununu katika shughuli zao za kila siku. Kadhalika, itachunguza mchango wa simu tamba katika kukuza na kuendeleza Kiswahili.