KISWAHILI KAMA NYENZO YA KUFUNDISHIA ELIMU YA URAIA KATIKA TAASISI ZA ELIMU NCHINI KENYA

Authors

  • Alex Umbima Kevogo
  • Mosol Kandagor Kandagor

Abstract

Lugha ya Kiswahili imepata hadhi kikatiba na kuwa lugha ya taifa na lugha rasmi nchini Kenya. Isitoshe, Kiswahili ndiyo lugha inayotumiwa na Wakenya wengi kwa ajili ya mawasiliano yao kila siku. Katiba ya Kenya inatambua umuhimu wa lugha ya Kiswahili kama chombo cha kukuzia umoja, wiano na utangamano wa kitaifa. Dhima ya Kiswahili kama lugha inayowaungunisha Wakenya wanaotoka katika maeneo na matabaka mbalimbali kitaifa haiwezi kusisitizwa bali inaeleweka wazi. Kutokana na uelewa huu, tunahoji kuwa lugha ya Kiswahili pamoja na hadhi yake kikatiba, inaweza kutumiwa kama wenzo wa kufundishia na kujifinzia elimu uraia vyuoni na shuleni. Elimu uraia ni msingi wa kujenga mihimili ya uzalendo na utaifa miongoni mwa wanafunzi wanaoibuka kutoka sehemu mbalimbali za taifa. Tunahoji pia kuwa Kiswahili ni chombo thabiti kinachoweza kutekeleza jukumu hili kwa ajili ya uwezo wake wa kuwaleta pamoja Wakenya. Msimamo wetu ni kuwa haiwezekani kufundisha masuala ya utaifa na uraia kwa lugha nyingine ambayo si ya taifa. Baadhi ya masuala muhimu yanayoweza kufundishwa kupitia kwa Kiswahili ni yale yanayohusu wiano wa kitaifa, uzalendo, katiba, serikali, utawala, ugatuzi wa mamlaka, demokrasia, haki za kibinadamu, uhifadhi na utunzaji wa mazingira, umoja na utangamano, usuluhishaji migogoro kwa njia ya amani na taathira za ufisadi. Makala hii basi inalenga kuonyesha umuhimu wa kutumia Kiswahili kutekeleza kazi hii na changamoto zinazoweza kuibuka kutokana na hali hiyo.

Chakama

Downloads

Published

2022-04-12

Issue

Section

Journals